DOGO ASLAY AWATENGENEZEA MJENGO WAZAZI WAKE
Msanii anayekuja kwa kasi kunako gemu la muziki wa kizazi kipya
Bongo, Aslay isihaka ameanza kuwaporomoshea mjengo wa maana wazazi wake,
eneo la Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam, Over The Weekend
inakujuza.
Akipiga stori na mwandishi wetu, dogo huyo anayesumbua na ngoma zake
kama Naenda Kusema na Uwe Nami, alisema ameamua kuwajengea wazazi wake
baada ya kuona wananyanyasika sana kwenye nyumba za kupanga.
“Mungu amenipa kipaji ili niwasaidie wazazi wangu kwa hiyo kila
nitakachokipata kwa sasa nitakielekeza kwenye nyumba hiyo iliyopo Gongo
la Mboto. Namshukuru sana Mkubwa Fella kwani yeye ndiyo anayenisimamia
kisanii na mafanikio haya yamechangiwa naye kwa kiasi kikubwa,” alisema
Aslay.
Category: celebrity
0 comments