Home �
� machafuko yatanda Zanzibar
Unknown |
Friday, October 19, 2012 |
0
comments
Taarifa kutoka visiwani Zanzibar nchini Tanzania zinasema kuwa, hali ya
usalama visiwani humo bado sio shwari kufuatia kutoweka katika hali ya
kutatanisha kiongozi wa Jumuiya ya Kiislamu ya Uamasho Sheikh Farid Hadi
Ahmed. Hali ya taharuki na machafuko ilianza kushuhudiwa katika maeneo
ya mkoa wa Mjini Magharibi kisiwani Ungauja hapo jana baada kuenea
taarifa za kukamtawa na kutekwa nyara na watu wasiojulikana Sheikh Farid
ambaye pia ni msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa askari mmoja wa kikosi cha kutuliza ghasia
cha FFU ameuawa kwa kupigwa mapanga na kukatwa kichwa na watu
wasiojulikana huku kukishuhudiwa pia vitendo kadhaa vya uhalifu ikiwa ni
pamoja na kuchomwa moto nyumba za wageni, maskani ya CCM ya Kisonge
mjini Unguja, maeneo ya biashara na hata mali za wananchi. Katika hali
ambayo vyombo vya usalama vinayahusisha matukio hayo na wafuasi wa
Uamsho, Katibu wa jumuiya hiyo Sheikh Abdullah Said amekanusha tuhuma
hizo na kusema kwamba wafuasi wa taasisi hiyo ya Kiislamu hawahusiki na
vitendo hivyo. Taarifa zaidi zinasema kuwa, machafuko hayo yanashuhudiwa
zaidi katika maeneo ya Darajani, Michenzani, Muembeladu, Magomeni na
Amani. Wakati huo huo Kamishna wa Polisi Zanzibar Mussa Ali Mussa
amesema kuwa, Sheikh Farid amepotea katika hali ya kutatanisha, na
kwamba hadi sasa juhudi za kumtafuta bado zinaendelea.
Category:
About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!
0 comments