Pembe za ndovu kuuzwa soko la Kimataifa
Serikali ya Tanzania inakusudia kuanzisha upya jaribio lake la kuuza
pembe za ndovu katika soko la kimataifa na imeahidi kuanza majadiliano
ya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na utalii ili kupata idhini
ya uuzaji wa rasilimali hiyo.
Hatua hiyo inakuja baada ya jaribio lake la kwanza kugonga mwamba
wakati wa mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa uliofanyika huko Doha
baada ya nchi wanachama kupinga hatua hiyo.
Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zilizima jaribio la awali la
Tanzania kwa madai hatua hiyo ingechochea kwa sehemu kubwa kushamiri kwa
ujangili wa pembe za ndovu. Hata hivyo Naibu Waziri wa Mali asili na
Utalii, Lazaro Nyalandu ametupilia mbali hoja hiyo akisema kuwa nia ya
Tanzania kuuza pembe hizo iko pale pale.
Mara hii Tanzania inakusudia kufanya majadiliano ya kina na Umoja wa
Mataifa kabla ya kuanza kikao kingine kilichopangwa kufanyika baadaye
huko Hongkong ambacho kitawashirikisha wajumbe wale wale waliijitokeza
kwenye kikao kilichopita cha Doha.
Duru za kimataifa zinasema kuwa mahitaji ya bidhaa zitokanazo na
pembe za ndovu zimeongezeka huku nchi za mashiriki ya mbali ikiwemo
China na Japan zikishika nafasi ya juu.
Category:
0 comments